Monday 22 May 2017

KIONGOZI WA MBIO ZA MENGE WA UHURU KITAIFA AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI NA WANANICHI KWA MIRADI YENYE TIJA.



Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2017, ndugu Amour Hamad Amour akiongea na wananchi wa chiwale baada ya kuweka jiwe la msingi katika mradi wa ujenzi wa  jengo la wodi kwa ajili ya akina mama na watoto  katika kituo cha afya cha chiwale kilichopo  kata ya chiwale Halmashauri ya Wilaya ya Masasi , wakati wa mbio za Mwenge wa Uhuru tarehe 14.05.2017 katika halamshauri hiyo.
Mkimbiza mwenge kitaifa ndugu Bahati Lugodisha akipata maelezo kwa moja ya kikundi cha wanawake na vijana wakati akikagua shughuli mbalimbali za vikundi hivyo siku ya  mbio za wenge wa uhuru katika Halmashauri ya Wilaya ya Masasi tarehe 14.05.2017 katika kata ya lukuledi.


Wananchi wa kijiji cha Mpindimbi  jatika halmashauri ya wilaya ya masasi wakiwa wamekusanyika eneo lilipojengwa tanki la maji  ambalo ni sehemu ya Mradi wa maji  wa Mpindimbi -shaurimoyo  wakati wa uwekaji wa jiwe la msingi katika mradi huo na Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2017, ndugu Amour Hamad Amour siku ya  mbio za wenge wa uhuru  tarehe 14.05.2017
Moja ya mradi uliozinduliwa na mbio za mwenge wa uhuru tarehe 14.05.2017 na Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2017, ndugu Amour Hamad Amour



Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2017, ndugu Amour Hamad Amour  akiweka jiwe la msingi katika mradi wa ujenzi wa  jengo la wodi kwa ajili ya akina mama na watoto  katika kituo cha afya cha chiwale kilichopo  kata ya chiwale Halmashauri ya Wilaya ya Masasi , wakati wa mbio za Mwenge wa Uhuru tarehe 14.05.2017 katika halamshauri hiyo.





Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa mwaka 2017 ndugu Amour  Hamad Amour amewapongeza viongozi na wananchi wa halmashauri ya wilaya ya masasi kwa kuanzisha na kusimmaia  miradi mizuri na yenye tija kwa wananchi  kama serikali ya awamu ya tano inayosisitiza juu ya uanzishaji  wa miradi ambayo inalenga kutoa huduma kwa wananchi ikiwemo elimu,afya na miradi ya kukuza uchumi . 

Amour alitoa pongezi hizo  wakati wa kukagua, kuzindua na kuweka mawe ya msingi kwenye miradi mitano yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni mbili wakati wa mbio za mwenge wa uhuru wilayani humo tarehe 14.05.2017  kwa kushuhudia ubora wa miradi hiyo ambayo inalenga kutatua kero kwa wananchi.

Amour aliwaeleza viongozi na wananchi kwa ujumla kuwa serikali ya awamu ya tano inalenga kuboresha huduma mbalimbali kwa wananchi ikiwemo afya, elimu na kukuza uchumi kwa kushiriki shughuli za uzalishaji mali  kupitia viwanda vidogovidogo na vikundi wa ujasiliamali.

Amour alifafanua kuwa utekelezaji  mzuri wa miradi ambayo inatatua moja kwa moja kero za wananchi itarahisisha wananchi kuutekeleza ujumbe wa mwenge kwa mwaka 2017 usemao “shiriki katika uchumi wa viwanda kwa maendeleo ya nchi yetu” maana kama watu watakuwa na uhakika wa kupata huduma za afya, maji na kuwa na kuwezeshwa kukuza uchumi ni dhahiri kuwa tutakuwa tumeitekeleza kwa vitendo dhana ya Tanzania ya viwanda.

Mwenge ukiwa wilayani masasi uliweza kupitia miradi ya ujenzi wa wodi ya akina mama na watoto katika kituo cha afya cha chiwale, ujenzi wa ofisi ya chama msingi cha chamali kilichopo lukuledi,mradi wa maji wa mpindimbi, soko la kisasa la mazao ya bustani kata ya chiwata na kugawa hundi kwa vikundi vya wanawake na vijana.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi bibi Changwa Mkwazu akipokea Mwenge wa Uhuru tayari kwa ukimbiza katika eneo lake

No comments:

Post a Comment