Katibu Tawala wa Wilaya ya Masasi Azizi Fakiri (aliyesimama) akifungua kikao cha TRA na watendaji wa kata, vijiji na Mitaa Wilaya ya Masasi jana tarehe 05.03.2019 katika ukumbi wa Nursing Mkomaindo kuhusu kodi ya Majengo.
Mamlaka ya Mpato
Tanzania (TRA) Wilayani masasi,
imewaomba watendaji wa kata, vijiji na mitaa katika Halmashauri ya wilaya na
mji Masasi kusaidia ukusanyaji wa kodi ya majengo katika maeneo yao ili kufanikisha
ukusanyaji wa mapato ya serikali kupitia chanzo hicho.
Akizungumza katika
kikao cha TRA na watendaji hao, Afisa mapato wa TRA Mkoa wa Mtwara Edwin Nkinga alisema, kodi ya majengo inatozwa kwa nyumba zilizopo
katika maeneo yote yaani kuanzia ngazi ya vijiji, mitaa na kata ndio maana
watendaji wanahusika moja kwa moja kutambua nyumba zote zilizopo katika maeneo
yao ili zilipiwe kodi kama sheria inavyoelekeza .
Nkinga alieleza kuwa “Kikao hiki kinalenga kuwaelimisha
nyinyi watendaji ili muweze kujua wajibu na majuku yenu katika ukusanyaji wa kodi za majengo ambapo
majengo yanayotozwa kodi ni yale yanayotumika”
Nkinga alifafanua kuwa,
Sheria ya kodi ya majengo inataja kiasi cha kodi kuwa ni shilingi 10,000 kwa nyumba za kawaida 20,000 kwa majengo ya ghorofa maeneo ya
vijijini na 50,000 kwa majengo ya
ghorofa maeneo ya mijini.
Aidha Nkinga alieleza
kuwa baadhi ya majengo yanapata msamaha wa kodi yakiwemo majengo yanayotumiwa
na Taasisi za Umma, majumba ya makumbusho au maktaba, majengo ndani ya
makaburi, nyuma zilizoezekwa kwa nyasi na za udongo
Watendaji wa kata, vijiji na mitaa wakiwa kwenye kikao
Alisema watendaji hao
wanatakiwa kusimamia ukusanyaji wa kodi za majengo katika maeneo yao kwa
kutumia mfumo wa bili za majengo kutoka TRA kwa kutambua nyumba zote zilizopo
kwenye maeneo yao kwa kujaza fomu kila mwaka ili kutambua idadi ya nyuma
zilizopo na hatimaye ziweze kuliiwa kodi
kulingana na hadhi ya jengo husika.
Kodi za majengo ni
chanzo kingine cha mapato ya serikali, hivyo watendaji wote wanatakiwa kwa ajili ya nyumba zote zinazostahili kulipa
kodi kwenye daftari la makazi katika maeneo yao.
Watendaji wa kata, vijiji na mitaa wakifurahia jambo kwenye kikao
Alisema sheria ya utoaji kodi ya majengo ya
mwaka 1983 imeainisha maeneo yanayotozwa kodi ya majengo kuwa ni Halmashauri za
miji, majiji, manspaa na wilaya.
Awali kodi za majengo
ilikuwa inakusanywa na Halmashauri zote nchini, lakini mwaka 2016 kupitia bunge
la bajeti serikali ilirekebisha sheria kodi ya majengo na kuipa TRA jukumu la
kukadilia,kukusanya na kuhesabu kodi ya majengo katika halmashauri zote nchini.
Aidha, alisema kuwa kwa atakae kaidi kulipa kodi kwa wakti
atachukuliwa hatua ikiwemo kulipa riba
kama adhabu, kufikishwa mahakamani
au kukamatiwa mali zake na kuuzwa ili kulipa kodi anayodaiwa.
No comments:
Post a Comment