Monday 22 May 2017

MATUKIO KATIKA PICHA MWENGE WA UHURU 2017 HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI TAREHE 14.05.2017

 Mwenge wa Uhuru ukiwa kwenye eneo la makabidhiano katika kijiji cha Nanyindwa kata ya Chiwale tayari kwa kuanza kukimbizwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Masasi.
 Kati Waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi wakiushangilia mwenge eneo la mapokezi
  Waheshimiwa madiwani wengine wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi  wakiushangilia mwenge eneo la mapokezi
 Mwanakikundi akitoa maelezo mbele ya mkimbiza mwenge kitaifa ndugu Bahati Lugodisha eneo la lukuledi kabla ya kukabidhiwa hundi za mikopo.
 Wakimbiza mwenge kitaifa wakiwa katika picha ya pamoja na wananfunzi wa shule maalumu ya lukuledi wenye ulemavu wa kutokusikia

 Viongozi na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi wakiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Masasi mhe. Selemani Mzee wakiwa kwenye eneo la kukabidhi mwenge wa uhuru wilaya ya Newala baada ya kumaliza kuukimbza katika Wilaya ya Masasi.


Watu wakicheza wakiwa wanasubilri kukabidhiwa Mwenge wa Uhuru



 

KIONGOZI WA MBIO ZA MENGE WA UHURU KITAIFA AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI NA WANANICHI KWA MIRADI YENYE TIJA.



Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2017, ndugu Amour Hamad Amour akiongea na wananchi wa chiwale baada ya kuweka jiwe la msingi katika mradi wa ujenzi wa  jengo la wodi kwa ajili ya akina mama na watoto  katika kituo cha afya cha chiwale kilichopo  kata ya chiwale Halmashauri ya Wilaya ya Masasi , wakati wa mbio za Mwenge wa Uhuru tarehe 14.05.2017 katika halamshauri hiyo.
Mkimbiza mwenge kitaifa ndugu Bahati Lugodisha akipata maelezo kwa moja ya kikundi cha wanawake na vijana wakati akikagua shughuli mbalimbali za vikundi hivyo siku ya  mbio za wenge wa uhuru katika Halmashauri ya Wilaya ya Masasi tarehe 14.05.2017 katika kata ya lukuledi.


Wananchi wa kijiji cha Mpindimbi  jatika halmashauri ya wilaya ya masasi wakiwa wamekusanyika eneo lilipojengwa tanki la maji  ambalo ni sehemu ya Mradi wa maji  wa Mpindimbi -shaurimoyo  wakati wa uwekaji wa jiwe la msingi katika mradi huo na Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2017, ndugu Amour Hamad Amour siku ya  mbio za wenge wa uhuru  tarehe 14.05.2017
Moja ya mradi uliozinduliwa na mbio za mwenge wa uhuru tarehe 14.05.2017 na Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2017, ndugu Amour Hamad Amour



Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2017, ndugu Amour Hamad Amour  akiweka jiwe la msingi katika mradi wa ujenzi wa  jengo la wodi kwa ajili ya akina mama na watoto  katika kituo cha afya cha chiwale kilichopo  kata ya chiwale Halmashauri ya Wilaya ya Masasi , wakati wa mbio za Mwenge wa Uhuru tarehe 14.05.2017 katika halamshauri hiyo.





Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa mwaka 2017 ndugu Amour  Hamad Amour amewapongeza viongozi na wananchi wa halmashauri ya wilaya ya masasi kwa kuanzisha na kusimmaia  miradi mizuri na yenye tija kwa wananchi  kama serikali ya awamu ya tano inayosisitiza juu ya uanzishaji  wa miradi ambayo inalenga kutoa huduma kwa wananchi ikiwemo elimu,afya na miradi ya kukuza uchumi . 

Amour alitoa pongezi hizo  wakati wa kukagua, kuzindua na kuweka mawe ya msingi kwenye miradi mitano yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni mbili wakati wa mbio za mwenge wa uhuru wilayani humo tarehe 14.05.2017  kwa kushuhudia ubora wa miradi hiyo ambayo inalenga kutatua kero kwa wananchi.

Amour aliwaeleza viongozi na wananchi kwa ujumla kuwa serikali ya awamu ya tano inalenga kuboresha huduma mbalimbali kwa wananchi ikiwemo afya, elimu na kukuza uchumi kwa kushiriki shughuli za uzalishaji mali  kupitia viwanda vidogovidogo na vikundi wa ujasiliamali.

Amour alifafanua kuwa utekelezaji  mzuri wa miradi ambayo inatatua moja kwa moja kero za wananchi itarahisisha wananchi kuutekeleza ujumbe wa mwenge kwa mwaka 2017 usemao “shiriki katika uchumi wa viwanda kwa maendeleo ya nchi yetu” maana kama watu watakuwa na uhakika wa kupata huduma za afya, maji na kuwa na kuwezeshwa kukuza uchumi ni dhahiri kuwa tutakuwa tumeitekeleza kwa vitendo dhana ya Tanzania ya viwanda.

Mwenge ukiwa wilayani masasi uliweza kupitia miradi ya ujenzi wa wodi ya akina mama na watoto katika kituo cha afya cha chiwale, ujenzi wa ofisi ya chama msingi cha chamali kilichopo lukuledi,mradi wa maji wa mpindimbi, soko la kisasa la mazao ya bustani kata ya chiwata na kugawa hundi kwa vikundi vya wanawake na vijana.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi bibi Changwa Mkwazu akipokea Mwenge wa Uhuru tayari kwa ukimbiza katika eneo lake

Friday 31 March 2017

WANAWAKE WAJENGEWE UWEZO KUELEKEA TANZANIA YA VIWANDA


Mgeni rasmi Bi.Eufrosina Chikojo (Afisa Tawala (W) Masasi akiwahutubia wananchi (hawapo kwenye picha) kwenye maadhimisho ya siku ya  wanawake duniani 2017 yaliyofanyika kiwilaya katika kijiji cha Lukuludi B.


Bi. Eufrosina Chikojo, Afisa Tawala(W) masasi akikagua vikundi vya ujasiriamali kwenye maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yaliyofanyika katika kijiji cha Lukuledi B siku ya tarehe 08.03.2017


Bi. Eufrosina Chikojo, Afisa Tawala(W) Masasi  akikabidhi hundi za mikopo kwa vikundi vya wajasiliamali vilivyopo kata ya lukuledi  kwenye maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yaliyofanyika katika kijiji cha Lukuledi B siku ya tarehe 08.03.2017
 Bi. Eufrosina Chikojo, Afisa Tawala(W) Masasi   akiendeea kukabidhi hundi za mikopo kwa vikundi vya wajasiliamali vilivyopo kata ya lukuledi

Thursday 30 March 2017

MAAFISA HABARI SERIKALI WAMETAKIWA KUTUMIA TOVUTI KUTOA TAARIFA SAHIHI KWA UMMA.




 Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mheshimiwa Evod Mmanda (wa tatu kulia) akizindua moja ya Tovuti iliyotengenezwa siku ya uzinduzi wa tovuti za serikali  zilizotengenezwa kwa udhamini wa Mradi wa uimarishaji wa mifumo ya sekta ya umma (PS3) kwa mikoa ya Mtwara, Lindi na Ruvuma tarehe 27 machi, 2017 katika ukumbi wa Tiffany Diamond Hotel

 Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mheshimiwa Evod Mmanda (aliyevaa Tai) akitoa maelezo maafisa Habari na Tehama baada ya kuzindua Tovuti za serikali zilizotengenezwa kwa mikoa ya Mtwara, Lindi na Ruvuma katika ukumbi wa Tiffany Diamond Hotel machi 27, 2017 (wa kwanza kulia ni kiongozi wa wawezeshaji ndugu Edgar Mdemu


Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mtwara mheshimiwa Evod Mmanda (wa tatu kulia) akiwa kwenye picha ya pamoja na wawezeshaji wa mafuno ya utengenezaji wa Tovuti za serikali
Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mtwara mheshimiwa Evod Mmanda (wa tatu kulia) akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya  maafisa Habari na Tehama  waliowezeshwa kutengeneza tovuti za taasisi zao.


Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mtwara ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Mheshimiwa Evod Mmanda amewataka  maafisa habari wa taasisi za serikali kuhakikisha wanatumia tovuti za serikali zilizotengenezwa kutoa taarifa sahihi na kwa wakati ili kuepusha changamoto ya upotoshaji taarifa mbalimbali za serikali kwa umma.

Mmanda aliyasema hayo wakati wa kufunga mafunzo ya siku saba ya uanzishaji wa Tovuti za serikali yaliyofanyika katika ukumbi wa Tiffany Diamond Hotel na kueleza kuwa maafisa habari ndio wanawajibu wa kutoa taarifa sahihi kwa umma, hivyo viongozi wa Taasisi za Serikali hawatakiwi kuzuia taarifa muhimu kwa wananchi kuingizwa kwenye Tovuti ili kuimarisha utawala bora unaozingatia uwazi na uwajibikaji kwa umma. 

Mmanda aliongeza kuwa kupitia tovuti hizo wananchi na wadau  wataweza kupata fursa ya kuandika au kutoa malalamiko yao moja kwa moja kwenye tovuti ya taasisi husika na kupata majibu kwa wakati bila kusumbuka kwenda ofisi za Taasisi hiyo hali ambayo itapunguza gharama na upotevu wa muda katika kupata huduma wanayotaka.

“Mnapaswa kufahamu kuwa upatikanaji wa taarifa kwa umma ni suala la kisheria, hivyo uwekaji wa taarifa kwenye tovuti za kutoa taarifa na kutangaza fursa mbalimbali  za uwekezaji zilizopo ni la lazima sio utashi wa mtu ni lazima taarifa hizi zihuishwe kila mara ili ziendane na wakati”  aliagiza Mmanda.

Aidha Mmanda alieleza kuwa Uwekaji wa taarifa za taasisi kwenye tovuti unaweza kuwasaidia  wawekezaji  kujua fursa zilizopo katika taasisizetu kwani atakuwa na uwezo wa kufahamu  awekeze kwenye nini na kwa kiasi gani ili awe kupata faida. 

Kwa Upande wake Mkuu wa timu ya wawezeshaji, Edgar Mdemu amesema mradi huo unaodhaminiwa na USAID umezindukiwa leo kitaifa mjini Dodoma na kwamba wanatarajia matumizi ya Tovuti yatasaidia kuimarisha utawala bora na ushirikishwaji  wa raia katika utekelezaji wa shughuli za serikali kwa uwazi.

Mafunzo ya utengenezaji wa Tovuti yalifunguliwa Machi 20 na kufungwa Machi 27 ambapo kitaifa zoezi la ufungaji limefanyika mjini Dodoma.Uimarishaji wa mifumo ya sekta za umma unaofadhiliwa na shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Marekani (USAID) ulianza mwaka 2016 na utadumu kwa miaka mitano (5) ambapo jumla ya Halmashauri 93 katika mikoa 13 ya Tanzania bara pamoja na serikali kuu zitanufaika.
Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mtwara mheshimiwa Evod Mmanda  akiitoa hotua wakati ya kufunga mafunzo ya utengenezaji wa tovuti za serikali  kwa mikoa ya Mtwara, Lindi na Ruvuma  na  kuzizindua rasmi.